Wednesday, 7 January 2015

OYAA PANYA ROAD, MNAJUA MNATUZINGUA WANA!


NI kwa blesi za Saa God makachaa tunamiti wansi ageini katika kijiwe chetu cha kujipa maraha, ama nini? Najua kitu cha mwezi dume, apecha alolo ndo kinasogea kwa mbaliii. Makidi wanataka kwenda skonga, fulu kutaka mazagazaga ya skuli nini na nini, shigidishida!

Mbaya zaidi wao hawajui kama jua limewakia mifukoni, mifuko imetoboka chezea mbishe za Sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya! Wao wanakomaa tu ili watimize wajibu wao wa kupiga msuli. Jichangechange kama vipi mwezi dume utapita na laifu litakaa kwenye mstari.

Tukirudi kwenye mastori yetu ya tauni, masela wa Panya Road ndiyo habari ya mujini. Wanawafanya maraia waishi kwa fasi ya uoga fulu stresi utadhani wako Dafuu au Iraki. Baa zote mastori ni Panya Road, vijiwe vyote ishu ni hiyohiyo.

Enewei ngoja niwape mchapo mmoko wa mwanangu Wile. Kama unavyojua tena mwezi dume unaendelea lakini mwana akakamata mchuchu wake wa longi taimu, aliulia taimingi kinoma lakini siku hiyo ukaingia kingi.

Huku na huku nini na nini baada ya kumtwangia mafoni, wakamiti katika baa moko iliyopo maeneo ya Sinza Kijiweni. Nisiwafiche wazazi, mtoto ni mtoto kweli, ana hoja kama vile kachorwa.
Mwana akachili naye katika kona f’lani yenye kitu cha mwanga hafifu kama unavyojua tena engo za malovee zinavyohusika.

Mdogomdogo kama songi la Diamond, jamaa akamuagizia kitu chupa kubwa lenye kilevi. Yeye akavuta Konya kubwa akawa anamiksi na maji makubwa huku mtoto mkaree akifyonza asteaste mvinyo wake. Muziki laini ulikuwa ukichombezachombeza, kinywaji kikaanza kufika mahali yake, wakaagiza manyamanyama si unajua tena pombe dawa yake kujichana? Chukua hiyo!

Stori za kuamsha hisia za malovee zikawa zinashuka pale kati, ghafla bin vuu masela wa meza ya mbele wakaibuka na kuanza kutimua mbio, mwana akatahamaki kutaka kujua nini kinaendelea, mubebizi ukachomoka nduki.

Mwana akasikia; “Panya Road...Panya Road...Panya Road.” Kusikia hivyo, mwana akasepa, pale mezani akaacha pochi ya mubebizi, simu zake za kutachi kama tatu akakimbilia toileti ya kike.
Baada ya dakika kama tano hivi, hali ikatulia na waliporudi katika meza yao wakakuta wana wamesafisha kila kitu, pamebaki peupeee!

Mwana stimu zote za mitungi zikakata, hakuwa na hamu tena ya kuponda raha. Alikuwa na mtonyo kwenye waleti ikabidi amsalimishe mtoto homu kwao na yeye akatimba zake magetoni akapindua.
Kitu cha msako ndo kikaanza kusanuka kitaani. Big up kwa Afande Suleiman Kova kozi naiti ileile aliingia kitaani na kuanza kuwatilia timu makamanda wake waliokuwa wakipiga misele katika viunga mbalimbali vya jiji!

Kova alitisha kinomanoma baada ya kutimba kwenye Televisheni ya Taifa TIBISII na kuwaondoa shaka wanyamwei wote kwamba wambonji kwani mamwela kibao wapo mitaani wakipiga doria.

Olu in olu, masela kitaani tunatakiwa kujikontroo wenyewe na michongo kaa hii ya Panya Road ni mizinguo. Washua ambao mnajua makidi wenu wanapiga hizo mbishe ni bora mkawaonya kabla hawajaingia kwenye mikono ya mwela wa Kova.Amani ya kitaa inaanza na mimi na wewe, kila mtu aplei pati yake na maisha yatakuwa burudani.

Sii yuu nexti wiki mazee, mzuka mwingi!

No comments:

Post a Comment